Welcome to pwaniraha blog please contribute by posting your comments on our blog, kindly note that abussive language is strictly not entertained. Thank you.
Welcome To Pwani Raha Blog; email us at "pwaniraha@gmail.com"

April 4, 2009

BENDI YA MALINDI IN NARDWAN SAFAA YAFANYA KWELI TRAVENTIN MAGOMENI

Bendi ya muziki wa Taarabu ya Zanzibar jana usiku wa kuamkialeo ilikonga nyoyo za wapenzi wa muziki huo pale walipofanya onyesho lao katika ukumbi Traveltine. Bendi hiyo iliyojizolea umarufu Afrika Mashariki na kati na huko katika bara la Ulaya, kundi hilo la muziki wa Taalabu lilianzishwa mwaka 1905 huko Zanzibar. Kiongozi wa kundi hilo Nasoro Issa Matona ambaye ni mtoto wa marehemu Issa Matona aliyefariki Dunia mwaka 2005 kwa kugongwa na gari wakati akie leke kwenye onyesho katika ukumbi wa Diamond Jubilee alisema kuwa kundi lao linapendwa sana kwa sababu ya kuimba nyimbo asilia zinazotokana na uafrika halisi. Kwa sasa kundi hilo lipo jijini Dar es Salaam ambapo wanategemea kufanya maonyesho kadhaa.













































1 comment:

Anonymous said...

Thnx 4 da pics, I was looking 4 them, I wish I was there.