
Mchezaji wa zamani wa Yanga ambaye msimu huu amesajiliwa na Africa Lyon zamani Mbagala makert Coastor Mumbala amesema leo kuwa tayari ameanza kuizoea jezi ya timu yake mpya. Akizungumuza na mwandishi wa habari hizi leo saa 2 asubuhi wakati walipokuwa wakifanya mazoezi katika uwanja wa uhuru alisema hakuondoka yanga kwa ubaya bali ni moja ya maisha ya mwana soka yeyote Duniani. Mumbala ambaye katika michuano ya Kili Taif Cup alikuwa kapteni wa timu yake ya mkoawa Mwanza alionyesha uwezo mkubwa sana katika michuano hiyo ambayo walimaliza kwa kushika nafasi ya nne.

Baadhi ya wachezaji wa timu ya Afican Lyon wakiwa mazoezini uwanja wa Karume leo.

Katika namba zote za mpira ugoli keeper ndio mgumu sana maana ukikaa benchi utabidi umuombee mwenzako aumie laa sivyo utaozea benchini. Cheki hawa magoli wanavyochangamka kila mmoja anataka aimiliki namba moja.
No comments:
Post a Comment