Welcome to pwaniraha blog please contribute by posting your comments on our blog, kindly note that abussive language is strictly not entertained. Thank you.
Welcome To Pwani Raha Blog; email us at "pwaniraha@gmail.com"

December 24, 2008

KUNDI LA SURVIVAL SISTERS KUTANGAZA ALBUM YAO YA YATIMA

Wasanii wa kundi la Survival Sister, wakipiga picha ya pamoja leo kutoka kushoto ni; Irene Malekela ( 24), Latifa Abdallaha (21) na Lucy Samson (24).









Kundi la Survival Sister ambalo linaundwa na akinadada watatu ambao ni walemavu Irene Malekala, Latifa Abdallah na Lucy Samson linatarajia kuitangaza albam yao ya Yatima ambayo ni album yao ya kwanza tangu kuanzishwa kwa kundi hilo. Akiongea katika mahojiano yaliyofanyika katika uwanja wa taifa wakati wasanii hao walipofika kushuhudi mchezo wa simba na URA ya Uganda,Irene alisema jamii inapaswa kutuunga mkono kwa kutusaidia kimawazo na kifedha,

Kikundi hicho kilianzishwa mnamo mwaka 2004 kipindi ambacho wasanii hao walikuwa wakisoma katika shule ya sekondari ya Jangwani, likijulikana kama QUEEN SISTERS na baadaye kuamua kubadili jina na kujiita Survival Sisters. Kundi hili si la kwanza kuwa na wasanii walemavu yawezekana wengi watakuwa wamesahau kulikuwa na kundi moja ambalo lilitokea kuteka nyoyo za wapenzi wa muziki wa kizazi kipya mnamo miaka ya 2001 hadi 2003.Kundi hilo lilijulikana kama kundi la Mabaga Fresh hivi sasa halijulikani liko wapi na hakuna anaye fuatilia.

No comments: