Welcome to pwaniraha blog please contribute by posting your comments on our blog, kindly note that abussive language is strictly not entertained. Thank you.
Welcome To Pwani Raha Blog; email us at "pwaniraha@gmail.com"

January 27, 2010

Offside Trick Watamba Sana Katika Anga Za Mduara (Chakacha)

Kundi la mduara la Offside Trick hivi karibuni limekuwa maarufu sana katika siku za karibuni na hii ni baada ya kutoa nyimbo zao mbili mpya zenye ujumbe tata ziitwazo; Samaki na Al bata. Kundi hili kutoka Zenji limekuwa likishirikisha wanamuziki maarufu kutoka huko kisiwani kama vile Mzee Yusuph na wengine.

Ndani ya video ya Al bata Mzee Yusuph anaonekana akiimba ilhali anaangilia bata huku mate yanamdondoka. Kama hauoni bata kwenye hiyo picha basi? "Kwaheri".

Moja ya ujumbe kwenye nyimbo hiyo ya Al bata unasema; "Nyama ya mbele ni kavu ya nyuma ina mafuta". Sasa sijui wanamaanisha nini ila sidhani kama ni mambo ya stori ya "Uncle Jambazi"

Pwani bila jahazi au kidau si pwani.

Mzee Yusuph Mwenywe.

6 comments:

Anonymous said...

Uncle jambazi ndio nani tena huyo.

Mbongo said...

vijana hawa wanatupa burudani ya mwaka, mimi binafsi wanaukonga moyo wangu shwadakta kabisa.

Anonymous said...

Stori ya ankal jambazi ni kali sana.

Anonymous said...

Nyimbo nzuri, sauti nzuri, maneno === matusi ===

siwezi kutizama video hiyo pamoja na dada , binti , baba yangu
maneno kama yule hanisi anasema "" nataka kutiwa ? "" au nyama ya ya nyuma ina mafuta ??? AIBU
NYIMBO HIZI NI VIGUMU KUSIKILIZWA NA HADHARA YA WATU WANAOJIHESHIMIWA

Anonymous said...

Jamani hii nyimbo ni aibu tupu...mdundo mzuri,sauti ya mwimbaji nzuri...LAKINI.....maneno ya nyimbo ni matusi matupu..khasara kubwa hii

Anonymous said...

Jamani hii nyimbo ni aibu tupu...mdundo mzuri,sauti ya mwimbaji nzuri...LAKINI.....maneno ya nyimbo ni matusi matupu..khasara kubwa hii