Welcome to pwaniraha blog please contribute by posting your comments on our blog, kindly note that abussive language is strictly not entertained. Thank you.
Welcome To Pwani Raha Blog; email us at "pwaniraha@gmail.com"

August 14, 2009

Madereva Ubungo Wagoma.

Asubuhi hi madereva wa mabasi yaendayo mikoani wamegoma. Tangu alfajiri leo asubuhi hakuna basi lolote lililotoka Ubungo bus Terminal. Madereva hawa wanadai kwamba dereva mwenzao alikuwa akiendesha mabasi ya Mohamed Trans aachiwe huru. Dereva huyu alihukumiwa kwenda miaka thelathini jela baada ya kusababisha ajali iliyoua mtu. Madereva hao wanasema kuwa ball joint ya basi hilo ilichomoka na kusababisha basi kupoteza mwelekeo hatimaye kusababisha ajali hiyo.

Hadi hivi sasa Hakuna basi lolote lililondoka Ubungo isipokuwa mabasi mawili ya Tahmeed ambayo huwa hayaingii kituoni Ubungo. Safari yake uanzia Kariakoo (Lumumba) na kuenda moja kwa moja hadi Tanga au Mombasa.

3 comments:

Anonymous said...

Kamanda Kova ndio amefika sasa hivi, wanaendelea na mazungumzo. Naona hapa FFU wapo maana kuna madereva fulani walitaka kuanza safari hapo awali matokeo yake wakala kichapo na madereva wanzao.

Anonymous said...

Kamanda Kova ndio amefika sasa hivi, wanaendelea na mazungumzo. Naona hapa FFU wapo maana kuna madereva fulani walitaka kuanza safari hapo awali matokeo yake wakala kichapo na madereva wanzao.

Anonymous said...

Mizengo Pinda ameshatatua tatizo magari yameanza safari kuelekea mikoani.